• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI WA ARDHI MANISPAA ZA JIJI WAJIKUTA KATIKA WAKATI MGUMU BAADA YA KUSHINDWA KUTOA MAJIBU KWA RC MAKONDA

Posted on: February 12th, 2018

Watendaji wa Ardhi wa Manispaa za Jiji la Dar es salaam leo wamejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kupata kigugumizi na kushindwa kujibu maswali ya msingi yaliyokuwa yakiulizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kuhusu idadi ya Migogoro ya Ardhi katika idara wanazoongoza na kusababisha baadhi yao kudondoka kwa kuzimia na kukimbizwa hospital.

Kitendo cha wakuu hao wa idara kushindwa kujibu maswali ambayo yamekuwa chanzo cha migogoro ya ardhi isiyoisha kimewakera Maelfu ya wananchi waliojitokeza kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kwaajili ya kujua hatma ya Malalamiko yao na kujikuta wakuomba RC Makonda kuwatumbua.

Kutokana na watendaji hao kushindwa kutekeleza majukumu yao RC Makonda ameagiza wakuu wa idara ya ardhi Manispaa za Ubungo na Ilala wapangiwe kazi nyingine kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Aidha RC Makonda amesimamisha shughuli zote za Mabaraza ya Kata Dar es salaam kuwakuwa hazina uwezo wa kusikiliza kesi na pia hawana wataalamu wa sheria kitendo kinachochangia Migogoro mingi ya Ardhi.

Kutokana na hilo RC Makonda amewataka Makatibu Tarafa kuanza kutembelea Mabaraza hayo kuanzia Jumatatu ya February 12.

RC Makonda amechukuwa uamuzi huo wakati wa kupokea Ripoti ya Malalamiko ya Wananchi waliodhulumiwa Haki zao ambapo zaidi ya Wananchi 11,652 walifika kwaajili ya kupata Msaada wa kisheria ambapo jumla ya malalamiko 3,373 yalipokelewa na kusikilizwa huku wananchi waliosikilizwa wakiwa ni 6,052 na ambao hawakupata fursa ya kusikilizwa wakiwa ni Wananchi 5600 ambapo leo RC Makonda ameandaa utaratibu wa kuhakikisha wote wanasikilizwa.

RC Makonda amesema idadi kubwa ya wananchi waliokimbilia kwake kutafuta haki ni tafsiri tosha kuwa baadhi ya watendaji hawasimami ipasavyo katika nafasi zao ambapo amewaagiza Wakurugenzi kuanza kupitia wasifu wa wakuu wa idara CV na kazi zote wanazofanya.

Ili kuhakikisha wanyonge walioporwa haki zao wanazipata pasipo kuvunja sheria RC Makonda amewasilisha kwa Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam Majina ya watu wenye michezo ya kudhulumu wananchi kwaajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Makonda ameagiza Watendaji kuhakikisha malalamiko yote ya wananchi ya Migogoro ya ardhi, Mirathi,Talaka, Madai, Makosa ya jinai, Masuala ya kazi, Ubakaji na utapeli yanafanyiwa kazi kabla ya mwezi April.

Aidha amewataka madalali wote wanaofanya kazi ya kutekeleza hukumu za Mahakama au Bank kufika ofisini kwake siku ya jumanne wakiwa na nyaraka za usajili.

Nao baadhi ya Wananchi waliofika kwenye mkutano huo wamefurahia hatua za RC Makonda katika kuwajali wananchi wanyonge ambapo pia wameshukuru mkutano huo umewasaidia kujua kwa undani masuala ya kisheria.

Aidha wamesema kuwa wanaamini kwa ujasiri RC Makonda wanafarijika kuona tabu waliyoipata kwa miaka mingi wakitafuta haki yao inaenda kupatikana.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa