• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

"Wananchi DSM Watakiwa Kujikinga na Magonjwa Yasiyoambukiza" RC Makalla.

Posted on: November 3rd, 2021

 

- Asema magonjwa yasiyoambukiza yanameongeza vifo zaidi 26% ya vifo vyote Nchini

- Abainisha wengi wa waathirika ni kuanzia miaka 35 na Chini ya miaka 60 tofauti na zamani ilikuwa ni watu wazima/wazee

- Aelekeza kila Wilaya ndani ya Mkoa kuhamasisha Wananchi kujikinga na Magonjwa yasiyoambukiza

- Asema Mkoa umeandaa KADI MAALUM itakazomuwezesha mwananchi kufuatilia AFYA yake

- Mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza DSM Dkt  Digna Riwa afafanua KADI hiyo

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo Novemba 3, 2021 amewataka wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kujikinga na Magonjwa yasiyoambukiza kwa kubadili mitindo ya Maisha.

Mhe Makalla ameyasema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Mikutano Arnatoglo-Ilala Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa magonjwa yasiyoambukiza yamekuwa yakiongezeka kwa kasi kiasi kwamba yameongeza vifo kwa zaidi ya 26% ya vifo vyote Nchini hivyo kupitia wiki ya Maadhimisho ya magonjwa yasiyoambukiza wananchi inayoanza  *Novemba 06, hadi 13, 2021, WAJITOKEZE kupima na kupata ushauri wa Kitaalam* ili waweze kubadili mitindo ya Maisha

Mhe Makalla amefafanua waathirika wengi siku hizi ni kuanzia umri wa miaka 35 na Chini ya miaka 60 tofauti na ilivyokuwa zamani magonjwa hayo yalikuwa yanawapata wazee/watu wazima zaidi ya miaka 60.

Aidha kupitia kauli mbiu ya mwaka huu Badili Mtindo wa Maisha " ameelekeza wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kusimamia zoezi hilo na kuhamasisha Wananchi katika maeneo yao katika Maadhimisho ya wiki ya magojwa yasiyoambukiza.

Sambamba na hilo Mkoa umeandaa KADI MAALUM zitakazogawiwa katika Wilaya zote za Mkoa ambazo zitamuwezesha mwananchi kufuatilia mwenendo wa Afya yake na badaye kumuona mtaalam husika, kama ni lishe atamuona mtaalam huyo.

Akifafanua KADI hiyo Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani na Tiba, na mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza Mkoa wa Dar es Salaam Dkt Digna Riwa amesema kupitia kadi hiyo itakuwa ni rahisi kufuatilia mwenendo wa afya mara baada ya kupima na kuweza kujua majibu ya afya yako kwa kuwa KADI hiyo inaelekeza kila hatua na nini cha kufanya.

"Mtu yeyote atakuwa na uwezo wa kufuatilia AFYA yake mahali popote hata kama hakuna mtaalam wa afya" Alisema Dkt Digna

Ifahamike kuwa Maadhimisho hayo ya wiki ya magojwa yasiyoambukiza* katika Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam yataambatana kufanya Mazoezi ya Kukimbia " Jogging" pia kupima na kupatiwa ushauri wa Kitaalam.

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla, NMB Wakabidhi Ticket kwa Viongozi wa Machinga na Bodaboda

    February 03, 2023
  • RC Makalla Apongeza Mahakama Utatuzi wa Migogoro kwa Usuluhishi

    February 01, 2023
  • RC Makalla Atoa Vipaumbele kwa Wakuu Wapya wa Wilaya za DSM

    January 31, 2023
  • RC Makalla Apiga Marufuku Biashara kwenye Barabara ya Mwendokasi Mbagala

    January 28, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akagua ujenzi wa Kipande cha SGR- kuingia Bandarini DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa