• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Mkalla: Watendaji Wote Tatueni Kero za Wananchi bila Kusubiri Ziara Majimboni.

Posted on: September 1st, 2021

# Aipongeza Wilaya ya Ilala kwa kutatua KERO za wananchi wake

# Asisitiza kukaa mpaka usiku katika kutatua KERO za wananchi MAJIMBONI

# Aahidi Kumleta Mhe. Rais katika uzinduzi wa Machinjio ya Kisasa

# Aendelea kuomba wananchi kudumisha Ulinzi na Usalama katika maeneo yao.

# Akerwa na Uuzwaji wa Biashara Holela Mashuleni, Barabarani na  Katika njia za watembea kwa miguu

# Awaelekeza DAWASA kuweka kambi Buguruni ili kuondoa changamoto ya maji taka


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla leo tarehe 1 Septemba ameendelea na ziara yake katika Wilaya ya Ilala Jimbo la Segerea.

Akiwa katika Jimbo Hilo Mhe.Mkuu wa Mkoa ameipongeza Wilaya hiyo kwa kupokea KERO chache kutoka kwa umati Mkubwa wa wananchi waliokuwepo ukilinganisha na Majimbo mengine aliyoyapitia.

Amesema " Ukiona uchache huo wa KERO za wananchi ujue Viongozi wake wanafanya kazi kubwa ya kutatua KERO zao vizuri" RC Makalla

Mhe. Makalla amesema kuwa katika Jimbo la Kawe alisikiliza na kutatua KERO za wananchi mpaka saa 11:00 Jioni aidha katika Jimbo la Kibamba alisikiliza na kutatua KERO za wananchi mpaka saa 1:00 Usiku

Awali Mkuu wa Mkoa alipokea KERO kutoka katika Jimbo hilo kuwa ni pamoja na Kero ya Barabara, Matatizo ya Urasimishaji, Matatizo ya Maji, Migogoro ya Ardhi, Malipo ya Fidia, Bonde la Mto Msimbazi, na Stendi ya Mabasi ya Muhimbili

Kuhusu uzinduzi wa Mradi Mkubwa wa Machinjio ya Kisasa ya Vingunguti uliotumia gharama ya shilingi *billioni 38* Mhe. Makalla ameahidi Kumleta Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuja na kuzindua Mradi huo kwani umekamilika kwa sasa, Mradi Mkubwa na unaenda kuifungua Dar es Salaam Kimataifa.

Wakati huo huo Mhe. Mkuu wa Mkoa ameendelea kuwaomba wananchi kudumisha Amani na Utulivu uliopo katika maeneo yao kwa kuwafichua wahalifu wote endapo wataonekana kuwepo katika maeneo yao.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amesema amekua akikerwa na Uuzwaji wa Biashara Holela Mashuleni, Barabarani, na katika njia za watembea kwa miguu kwani wanahatarisha Usalama wa watu kwa ujumla kwa kufanya Biashara maeneo hatarishi.

Kwa upande wa KERO ya majitaka yanayotiririka katika baadhi ya maeneo ya wakazi wa Buguruni Mhe. Mkuu wa Mkoa amewataka DAWASA kuweka kambi Buguruni ili kuondoa KERO hiyo

Serikali ya Awamu ya Sita kupitia Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan imeahidi kuukamilisha miradi yote iliyoanza kutekelezwa hivyo Awamu hii ya tatu ya DMDP tayari Billioni 3.8 zimeshatengwa ili kujenga Barabara katika Wilaya ya Ilala alisema  Mhe. Amos Makalla







Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa