• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Wanachi Wanahitaji Msaada wa Kuelewa Sheria na Mamlaka ya Serikali na Mahakama

Posted on: February 2nd, 2022

 

- Asema Wananchi bado wanaamini Serikali ni rufaa ya kesi zote walizoshindwa Mahakamani

-Abainisha uzoefu unaonyesha HAKI haijawahi kukubaliwa siku zote hukataliwa, hivyo wasikate tamaa

- Atoa wito Mahakama kujikita katika kutoa Elimu kwa Umma ili jamii iwe na Uelewa wa maswala ya Kisheria

- Apongeza Maboresho makubwa yanayofanywa, hasa matumizi ya Teknolojia ya Habari

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo Februari 2, 2022 ameshiriki kilele cha wiki ya Sheria Mkoa wa Dar es Salaam katika Viwanja vya Mahakama ya Kisutu akiwa Mgeni Maalum

RC Makalla akiongea na hadhara ya Wataalam wa sheria wakiwemo Waheshimiwa Majaji na Mahakimu  amesema wananchi WANAHITAJI zaidi msaada wa uelewa wa sheria na mamlaka ya Serikali na Mahakama kwa kuwa wanaamini Serikali ni Rufaa ya kesi zote walizoshindwa Mahakamani hivyo ni vema wakaelimishwa ili wapate uelewa.

Hata hivyo uzoefu unaonyesha kuwa aliyetenda kosa iwe ni kubaka, kuua na kesi nyingine yeyote anapokutwa na mkono wa Sheria hawezi kukubali mara zote husema nimebambikiwa kesi na kuendelea kutoa lawama ameonewa, hivyo Waheshimiwa Majaji na Mahakimu wasikate tamaa kazi yao ni ngumu waendelee KUTENDA HAKI

Aidha RC Makalla amesema wakati anazunguka katika majimbo kusikiliza kero za wananchi alibaini mamboo mengi lakini kwa upande wa uelewa wa wananchi juu ya mamlaka ya muhimili wa Mahakama na Serikali bado ni mdogo.

" Utakuta mwananchi anakuja mgogoro ambao tayari Mahakama inashughulikia au imetoa hukumu za kisheria, bado yeye atalazimisha Mhe Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya atengue huku akiamini Serikali ndio kila kitu" Alisema RC Makalla

Hivyo kutokana na uzoefu huo unaonekana kwa Jamii yetu ni vema sasa muhimili huu muhimu wa Mahakama kuelekeza nguvu kubwa au kujikita katika kutoa Elimu kwa Umma juu ya maswala ya Kisheria.

Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa amepongeza maboresho makubwa yanayofanywa na Mahakama hasa matumizi ya TEHAMA katika Utekelezaji wa majukumu kila siku kwa kuwa matumizi ya Teknolojia ya Habari yanasaidia kuondoa urasimu, rushwa, gharama, lakini pia ufanisi wa kazi kwa kuwa mashauri huweza kusikilizwa mahali popote mtu alipo.

RC Makalla ameahidi kuendelea kushirikiana na Mahakama katika nyanja mbalimbali kwa kuwa Kazi za Serikali hufanywa kwa kutegemeana

Ifahamike kuwa Maadhimisho ya wiki ya Sheria ni kiashiria cha kuanza kwa shughuli za kisheria kwa mwaka mpya 2022 kwa kuwa hutoa nafasi ya kutathimini yale yaliyofanyika mwaka iliopita ili kuwa na ufanisi zaidi wa muhimili huo muhimu wa Mahakama

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA AFUNGUA MKUTANO WA "AFRICA E- MOBILITY FORUM"

    March 21, 2023
  • RC Makalla Akabidhi Hundi ya Mikopo ya 10% zaidi ya Bilioni 4.6 Temeke Atoa Maagizo Matano

    March 20, 2023
  • RC Makalla Masoko Mapya Yatakayojengwa Washirikishwe Machinga na Viongozi wa Soko

    March 11, 2023
  • RC Makalla Aeleza Kishindo Cha Rais Dkt Samia Suluhu Miaka 2 DSM

    March 10, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akikagua Maendeleo ya Ujenzi na ukarabati wa Soko la Kariakoo
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa