• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Operesheni Awamu ya Tatu ya Wazalishaji na Watumiaji Mifuko ya Plastic iliyokatazwa Kuanza Mei Mosi

Posted on: April 14th, 2023

 

- Atoa Wiki Moja kwa NEMC na TBS kuweka ratiba ya kutoa elimu kwa Wananchi Wilaya zote za DSM.

- Aonya Bar na Kumbi za starehe zinazopiga mziki mkubwa na kusababisha kero kwa Wananchi

- Aseme kikao Cha leo kimetanguliwa Na kikao  Cha Vongozi wa Dini Kuhusiana na kero ya  kelele nyumba Za ibada kwenye makazi.

- Ataka Sheria, Kanuni na taratibu za NEMC kufuatwa

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam CPA, Amos Makalla ametangaza Kuanza kwa operesheni kabambe ya kukamata wazalishaji na Watumiaji wa Mifuko ya plastic iliyokatazwa kuanzia Mei Mosi ambapo amewataka Wananchi kuanza kuchukuwa tahadhari.

RC Makalla ameelekeza Baraza la uhifadhi na usimamizi wa mazingira NEMC kwa kushirikiana na TBS kuweka ratiba ya Siku za kutoa elimu kwenye Wilaya zote za Mkoa huo kabla ya Kuanza kwa operesheni hiyo Ili kujenga uelewa.

Hatua hiyo imekuja baada ya matumizi ya mifuko ya plastic iliyokatazwa Kuanza kurudi upya Licha ya Serikali kupiga marufuku.

Akizungumzia wakati wa mkutano wa udhibiti mifuko ya plastic, Kelele za mziki na mitetemo, RC Makalla pia amewataka Wamiliki wa Bar na Kumbi za starehe na Vyombo vya mziki kufuata na kuzingatia Sheria, Kanuni na miongozo ya Baraza la uhifadhi na usimamizi wa mazingira NEMC ili kuepusha kero ya Kelele za mziki kwa Wananchi.

Aidha RC Makalla amesema kumekuwa na malalamiko Makubwa ya uvunjifu wa Sheria kufuatia ongezeko la Bar na Kumbi Za starehe kwenye makazi ya watu ikiwa ni pamoja na upigaji mziki usiku mzima na kuathiri Wananchi.

Katika mkutano huo uliohusisha Viongozi wa mitaa, Masoko na wadau wa mazingira, RC Makalla ameelekeza Viongozi wa Serikali za mitaa kuchukuwa hatua ikiwa ni pamoja na kudhibiti utoaji vibali vya ujenzi kiholela.

Kwa mujibu wa sheria na Kanuni za NEMC makosa na adhabu kwa wanaokiuka Sheria ya kupiga mziki kwenye makazi ya watu ni faini ya shilingi milioni 2 mpaka milioni 10, kifungo Cha Miaka miwili jela au vyote kwa pamoja na Sheria inaruhisu upigaji mziki kuanzia Saa 12 asubuh mpaka Saa nne usiku kwa kiwango kilichoruhusiwa na kwa bar zinazokesha nao wamepewa taratibu za kufuata Ili kupewa kibali.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa