• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Awaeleza Viongozi wa Masoko DSM Kuwa Vyanzo vya Majanga ya Moto ni Uzembe

Posted on: April 29th, 2022

 .

RC Makalla akizima moto kwa kutumia kizima moto Anatoglo Mnazimmoja mara baada ya kumaliza kikao kazi cha mikakati ya mapambano dhidi ya majanga ya moto katika masoko


- Asema kila palipotokea Moto chanzo chake ni kujiunganishia umeme kiholela, kuacha maharage usiku na mateja kulala katika Masoko.

- Aagiza masoko yote yawe na fundi anayetambuliwa Na TANESCO. 

-  Aagiza Jeshi la Zimamoto kutoa Elimu ya kujikinga na majanga kwenye kila soko.

- Wakurugenzi Maafisa biashara waboreshe masoko, barabara, maji na kununua vizimia moto kila soko.

- Aagiza uongozi wa Masoko kuimarisha ulinzi wa Masoko.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla leo April 29 amefanya kikao Cha pamoja baina yake, Viongozi wa Masoko na Jeshi la Zimamoto na uokoaji kwa lengo la kutoa Elimu ya udhibiti wa Majanga ya Moto kwenye masoko ya Mkoa huo.

Uamuzi wa RC Makalla kuhitisha kikao hicho ni Kufuatia kuungua kwa baadhi ya Masoko ndani ya Muda ambapo ripoti za Kamati zinazoundwa kuchunguza zinaonyesha kuwa chanzo ni Uzembe wa watu kujiunganishia umeme kiholela na kinamama kuhinjika maharage kwenye majikoni usiku ili asubuhi wakute yameiva.

Kutokana na changamoto hiyo RC Makalla ameelekeza kila soko kuwa Vifaa vya kudhibiti moto na fundi wa umeme anaetambuliwa na TANESCO.

Aidha RC Makalla ameelekeza Jeshi la Zimamoto na uokoaji kuandaa ratiba ya kupita kila soko la Mkoa huo na kutoa Elimu ya kujikinga na majanga ya Moto.

Kuhusu changamoto ya uchakavu wa Masoko iliyolalamikiwa na Viongozi wa masoko, RC Makalla ameelekeza Kila Halmashauri kupitia Wakurugenzi na Maafisa biashara kuboresha Masoko, Barabara, Maji, Vyoo na kununua vizimia Moto.

Kwa upande wao Viongozi wa masoko Wamemshukuru RC Makalla kwa kuona tatizo lililopo na kuamua kuhitisha kikao Cha kupatia majibu changamoto ya Masoko kuuungua ambapo wameeleza kuwa kwa miaka mingi haijawahi kutokea kiongozi akahitisha kikao Kama hicho Cha kutoa Elimu ya kujikinga na majanga ya Moto hivyo kitendo alichofanya kimewapa matumaini makubwa.

Itakumbukwa kuwa hivi karibuni kumeibuka matukio ya kuungua moto kwa baadhi ya Masoko ikiwemo Soko la Kariakoo, Coca-cola, Karume, Mbagala na Soko la mchikichini.

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla, NMB Wakabidhi Ticket kwa Viongozi wa Machinga na Bodaboda

    February 03, 2023
  • RC Makalla Apongeza Mahakama Utatuzi wa Migogoro kwa Usuluhishi

    February 01, 2023
  • RC Makalla Atoa Vipaumbele kwa Wakuu Wapya wa Wilaya za DSM

    January 31, 2023
  • RC Makalla Apiga Marufuku Biashara kwenye Barabara ya Mwendokasi Mbagala

    January 28, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akagua ujenzi wa Kipande cha SGR- kuingia Bandarini DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa