• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla: Atembelea Wasafi na Clouds Media, Asisitiza Dar ni Salama

Posted on: August 26th, 2021

 

Mhe Amos Makalla akiwa studio za Clouds FM katika kipindi cha power breakfast mapema leo.


-Aelezea mkakati wake wa kuanza kusikiliza kero za wananchi katika majimbo ya pembezoni mwa Jiji, Agosti 30,2021 kuanza na Jimbo la Kawe

-Apongeza Jeshi la Polisi kwa kufanikiwa kumdhibiti mualifu aliyesababisha vifo vya askari 3 na mgambo mmoja eneo la Sarenda bridge Jana Septemba 25, 2021

-Abainisha dhamira yake ya kuwaondoa wafanyabiashara holela ili kuliweka Jiji safi kwa kuweka utaratibu mzuri ambao hautaathiri biashara zao

-Azungumzia suala la kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makala leo Agosti 26, 2021 amefanya ziara katika vituo viwili vya habari Wasafi na Clouds Media

Akiwa katika vituo hivyo alipata wasaa wa kutembezwa katika vyumba mbalimbali vinavyotumika katika uchakataji wa habari.

Mhe Makalla amevipongeza vituo hivyo kwa namna vinavyofanya kazi na kuahidi kufanya navyo kazi kwa kuwa tasnia ya habari ni mdau muhimu wa maendeleo.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kuanzia Jumatatu ambayo ni Agosti 30, 2021 anaanza kusikiliza kero za wananchi katika majimbo ya pembezoni ambayo ni Kawe, Kibamba, Mbagala na Segerea akianza na Jimbo la Kawe eneo la Tanganyika   Perkers huku akitoa rai kwa wananchi kujitokeza zoezi litaanza saa 2: 00 asubuhi na kutakuwa na timu wataalam wote

Mhe Makalla akizungumzia suala la usalama katika Mkoa amesema Mkoa uko salama wananchi waendelee kutekeleza majukumu yao ya kila siku, kwa upande wa tukio la jana amepongeza jeshi la Polisi kwa kumdhibiti mwalifu licha ya kuwa alifanikiwa kufanya mauaji ya watu 4 uchnguzi unaendelea ukikamilika ripoti itatolewa.

Sambamba na hilo Mhe Makalla amebainisha anavyo kwenda kukabiliana na wafanyabiashara holela pasipo kutumia nguvu, kwa sasa tayari mabango yanawekwa kuanisha maeneo ambayo hairusiwi kufanya biashara, ambapo kupitia zoezi hilo litasaidia kuufanya Mkoa kuwa safi.

Kwa upande wa miradi ya maendeleo amesema tayari ameshaelekeza kwa wakuu wa Wilaya katika Mkoa Salaam yake ni neno "MKUUU" tafsiri yake M- Mapato, K- Kero za wananchi, U- Ulinzi na Usalama, U- Usafi na U- Usimamizi wa miradi ya maendeleo,

"hivyo hizo herufi 5 lazima zisimamiwe vizuri kwa kila kiongozi na watumishi katika Mkoa wa Dar es Salaam" Alisema Mhe Makala

Mkuu wa Mkoa amesema amejipanga kuboresha fukwe zote ziwe kivutio cha utalii anaanza na Coco Beach pia yuko tayari kukutana chama cha wanamziki kuona namna bora ya kuboresha tasnia hiyo ya burudani.

Amesisitiza Wananchi kwenda kupata chanjo ya UVIKO-19 na kuendelea kuchukua tahadhari zote kwa kuwa ugonjwa huo upo.


Mhe Amos Makalla akiwa studio ya Wasafi FM katika kipindi cha Good Morning 

Matangazo

  • RATIBA YA KAZI YA MHE. RC MAKALLA KUANZIA 20 - 26 APRIL,2022 April 20, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Utamilifu (Mock) Mkoa wa Darasa la Saba - 2021 July 30, 2021
  • TAARIFA KWA UMMA BEI ELEKEZI YA MBOLEA March 30, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla Operesheni Panya Road Imekuwa na Mafanikio

    May 27, 2022
  • RC Makalla Asimamisha Shughuli za Uchimbaji Madini Boko - DSM

    May 26, 2022
  • Dar es Salaam Yaadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani

    May 24, 2022
  • DC Ilala Ataka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kuchukua Hatua kwa Wanaokaidi Maelekezo Wanayoyatoa

    May 19, 2022
  • Tazama zote

Video

Maelekezo ya RC Makalla juu ya Mapambano dhidi ya majanga ya moto katika masoko DSM.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa