• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Ataka Maeneo Wanayohama Wamachinga Yawe Safi

Posted on: October 20th, 2021

- Aagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kusimamia usafi ndani ya wiki moja kuanzia leo

- Awataka Watendaji wa Kata na Mitaa kuyalinda maeneo yasiwekwe vibanda tena

- Asema kila Taasisi ya Umma kulinda eneo lake

- Asisitiza kufikia Oktoba 30, 2021 hataki kuona kibanda chochote kwenye "Road Reserve"

- Ameendelea kupongeza uongozi wa Machinga DSM kwa kushirikiana na Serikali

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo Oktoba 20, 2021 amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi katika Mkoa wa DSM kuhakikisha maeneo yote ambayo Machinga wanahama yanafanyiwa usafi ndani ya Wiki moja kuanzia leo.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo wakati anaongea na waandishi wa habari katika Ukumbi wa mikutano Arnatoglo-Ilala Jijini Dar es Salaam.

Mhe Makalla amewataka Watendaji wa Kata na Mitaa kuyalinda maeneo katika Kata au mitaa yao, kwa kuwa wamachinga sasa wanahama kwenda maeneo sahihi waliyowapanga hatarajii kuona wafanyabiashara hao wanarudi tena katika maeneo ya awali wakati Mtendaji wa Kata au Mtaa husika yupo.

Mhe Mkuu wa Mkoa pia amezitaka Taasisi zote za Umma ambazo ziko katika Mkoa wa Dar es Salaam kulinda maeneo yake yasivamiwe tena na wafanyabiashara wadogo.

Mhe Makalla amesema ifikapo Oktoba 30, 2021 hataki kuona kibanda chochote kwenye "Road Reserve" ametolea mfano barabara ya Morogoro na Barabara ya Airport.

Aidha Mhe Makalla amebainisha ndani siku 12 alizoongeza ni matarajio yake *Mitaro na mifereji itakuwa wazi, Njia za watembea kwa miguu zitakuwa wazi na safi, hakutakuwa na wafanyabiashara walio mbele ya maduka ya wengine, Mitaa iwe safi na inapitika*

Sambamba na hilo Mhe Makalla amesema anamshukuru Mungu zoezi la kuwapanga wamachinga Vizuri linaendelea vema tena kwa mafanikio makubwa, amewashukuru wamachinga na kuupongeza uongozi wa wamachinga DSM kwa kujitambua na kushirikiana vizuri na Serikali ni imani yake kuwa DSM sasa inaenda kuwa safi na inayovutia.

Mkuu wa Mkoa amesema ukiangalia sababu kubwa inayofanya Dar es Salaam kuwa chafu ni biashara holela hivyo zoezi la kuwapanga vizuri wamachinga likikamilika atazindua rasmi kampeni ya usafi DSM

Dar es salaam safi na inayovutia inawezekana tuendelee kutoa Elimu kila mmachinga afanye biashara katika sehemu sahihi

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla, NMB Wakabidhi Ticket kwa Viongozi wa Machinga na Bodaboda

    February 03, 2023
  • RC Makalla Apongeza Mahakama Utatuzi wa Migogoro kwa Usuluhishi

    February 01, 2023
  • RC Makalla Atoa Vipaumbele kwa Wakuu Wapya wa Wilaya za DSM

    January 31, 2023
  • RC Makalla Apiga Marufuku Biashara kwenye Barabara ya Mwendokasi Mbagala

    January 28, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akagua ujenzi wa Kipande cha SGR- kuingia Bandarini DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa