• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Apokea Kero zaJumuiya ya Wafanyabiashara Dar es Salaam.

Posted on: May 16th, 2022

 

- Awakutanisha Pamoja Jumuiya ya wafanyabishara na Watendaji wa Serikali DSM wakiwemo TRA, Bandari, Uhamiaji na Jeshi la polisi

-Aongoza mjadala wa kuweka mazingira bora ya Kibiashara na Uwekezaji DSM, Atoa maagizo 7 ya Utekelezaji wa makubaliano yaliyofanyika

-Ampongeza Rais Samia kwa kuvunja rekodi kupandisha mishahara ya watumishi kwa 23.3%

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo Mei 16, 2022 amefanya kikao Kazi kwa kuwakutanisha pamoja Jumuiya ya wafanyabishara DSM pamoja na Watendaji wa Serikali na wadu wengine kwa lengo la kupokea Changamoto zao na kuweka mazingira rafiki ya Kibiashara na Uwekezaji kwa Masilahi Mapana ya Mkoa na Taifa kwa Ujumla

Kikao ambacho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Anatoglo Mnazimmoja Ilala-Jijini Dar es Salaam.

Akiongea wakati wa kikao hicho RC Makalla amesema pamoja mambo mengine anayosimamia Mapato ni kipaumbele kwake na namna mojawapo ya kupandisha mapato ni pamoja na kuweka mazingira rafiki ya Kibiashara pasiwepo na kero zinazokwamisha utendaji wa biashara.

Aidha RC Makalla ameyataja maeneo Makuu manne ya kero ambayo ni miongoni mwa kero  zilizowasilishwa kwake na Jumuiya ya wafanyabishara DSM.

Miongoni mwa kero hizo ni Ukamataji wa mizigo ya wafanyabishara hasa wa nje kero iliyoelekezwa TRA na Jeshi la polisi, Utoaji wa muda wa Vibali (Vissa) kwa wafanyabishara wa nje umekuwa ni siku 7 ambao hautoshelezi Kibiashara angalau ungesongezwa kuanzia siku 30-90

Vilevile Kero ya Ucheleweshaji wa mizigo Bandari na makadirio ya kodi kwa wafanyabishara sio rafiki

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa alitoa nafasi kwa Watendaji wa Serikali kutoa majibu ya kero zilizoelekezwa katika Mamlaka zao hususani kero zilizoko ndani ya uwezo wa taasisi kwa lengo la kuweka mazingira rafiki ya Wafanyabishara DSM.

RC Makalla baada ya kusikiliza majibu yaliyotolewa akatoa maagizo 7 kama ifuatavyo: Majibu yote yaliyo tolewa kwa Upande wa TRA, Bandari, Uhamiaji, yawekwe katika maandishi yafike Ofisini kwake Jumatano Saa 5:00 Asubuhi, Mkoa uwe tayari kimkakati kuhakikisha unaendelea kuchangia pato la taifa kwa kiwango kikubwa huku akitaka kuundwa kwa kamati ya kushughulikia masuala ya biashara itakayoongozwa na katibu Tawala Mkoa

Vilevile mabaraza ya wafanyabishara yafanyike katika Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam, Mamlaka za Udhibiti biashara kama Osha, Zimamoto, TBS na zingine kutoa nafasi nzuri na rafiki kwa wafanyabishara kufanya kazi zao, Mamlaka ya Bandari Tanzania kuwaandikia barua "Shipping Line" kufanya kazi kwa weledi mzigo ukiingia mara moja kupelekewa Bandari kavu, Uhamiaji kupeleka mapendekezo ya namna ya kuboresha utoaji wa "Vissa" kwa Kamishna Jenerali

Kwa Upande Ushuru wa huduma "Service Levy" RC Makalla ameagiza katibu Tawala ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati kuja na mapendekezo ya ni kifanyike

Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa wa DSM amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusikia kilio cha Siku nyingi cha watumishi wa Umma na kupandisha mishahara kwa alimia 23.3 na ametoa Rai kwa watumishi wote kutekeleza wajibu wao kwa kufanya kazi kwa bidii

Mhe Amos Makalla siku ya Jana Mei 15, 2022 ametimiza mwaka mmoja toka ateuliwe na Mhe Rais huku Mkoa ukiwa na mafanikio lukuki katika nyanya za Mapato, Ulinzi na Usalama, Kuwapanga vizuri Wamachinga, Kampeni Usafi , Usikilija wa kero za wananchi, Usimamizi wa kiwango cha juu miradi ya maendeleo, na Ukamilishaji kwa wakati Ujenzi wa madarasa na Anwani za Makazi

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA AFUNGUA MKUTANO WA "AFRICA E- MOBILITY FORUM"

    March 21, 2023
  • RC Makalla Akabidhi Hundi ya Mikopo ya 10% zaidi ya Bilioni 4.6 Temeke Atoa Maagizo Matano

    March 20, 2023
  • RC Makalla Masoko Mapya Yatakayojengwa Washirikishwe Machinga na Viongozi wa Soko

    March 11, 2023
  • RC Makalla Aeleza Kishindo Cha Rais Dkt Samia Suluhu Miaka 2 DSM

    March 10, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akikagua Maendeleo ya Ujenzi na ukarabati wa Soko la Kariakoo
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa