• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Akerwa Kusuasua Kwa Ujenzi wa Barabara Makongo Juu

Posted on: December 15th, 2021

 - Asema hajaridhizishwa na kasi ya Ujenzi atapeleka taarifa kwa Waziri mwenye dhamana

- Awahakikishia wakazi wa Makongo Juu kuwa yuko pamoja nao

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla amekagua maendeleo ya Ujenzi wa Barabara ya Ardhi, Makongo Juu Goba na kuonyesha kukerwa na namna mkandarasi anavyosuasua kukamilisha Ujenzi wa Barabara hiyo.

RC Makalla baada ya kukagua Barabara hiyo alipata wasaa wa kuongea na Wananchi ambao ni wanufaika wa mradi huo ambapo waliweza kumueleza kero zao zikiwemo, kuwepo kwa vifusi vya mchanga, Vumbi, kukosekana kwa mifereji ya maji, na fidia kwa kaya zilizobomolewa

Vilevile viongozi wa chama waliopewa nafasi ya kuzungumza mbele ya wananchi wameonyesha kutoridhishwa na mkandarasi anayetekeleza mradi huo wakimuomba Mkuu wa Mkoa kuingilia Kati.

Aidha RC Makalla amesema yeye binafsi ni Mara yake ya pili kutembelea mradi huo ambapo alipofika kwa mara ya kwanza na sasa haoni tofauti, hali inayomfanya kuamini mkandarasi huyo hana uwezo.

Hivyo kutokana na kusuasua uko anaenda kumpa taarifa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof Makame Mbarawa aje aitembelee Barabara hiyo na kutoa uamuzi kwa maslahi mapana ya Wananchi.

Sambamba na hilo Mhe Makalla amezipokea Changamoto zilizotolewa na wananchi na kuwahakikishia yuko upande wao yale yote ambayo yako ndani ya uwezo wake yatafanyiwa kazi kwa haraka.

Kwa Upande wa mhandisi wa Tanroad *Mwanaisha Rajabu amekiri mkandarasi wa mradi huo kuwa na kasi ndogo licha ya wao kama Tanroad kumueleza mara kea mara kuongeza kasi ya Utekelezaji wa Miradi.

RC Makalla ametoa RAI kwa wakandarasi wazawa kufanya kazi zenye ubora na kuzingatia muda ili Serikali isione sababu ya kutumia wakandarasi wa Nje

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla, NMB Wakabidhi Ticket kwa Viongozi wa Machinga na Bodaboda

    February 03, 2023
  • RC Makalla Apongeza Mahakama Utatuzi wa Migogoro kwa Usuluhishi

    February 01, 2023
  • RC Makalla Atoa Vipaumbele kwa Wakuu Wapya wa Wilaya za DSM

    January 31, 2023
  • RC Makalla Apiga Marufuku Biashara kwenye Barabara ya Mwendokasi Mbagala

    January 28, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akagua ujenzi wa Kipande cha SGR- kuingia Bandarini DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa