• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC MAKALLA: AELEKEZA MAMBO 9 UTOAJI MIKOPO YA VIKUNDI

Posted on: September 30th, 2022

 

RC Makalla amepokea taarifa ya mikopo ya asilimia kumi 10% Mkoa wa Dar es Salaam kupitia Mkutano uliowajumuisha Viongozi na Watendaji wa Mkoa wakiwemo Sekretarieti ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Mameya, wataalam wa maendeleo ya Jamii, waweka Hazina na wadau mbalimbali kutoka katika majukwaa ya Kuwezesha Wananchi Kiuchumi katika Ukumbi wa Arnatoglo Mnazimmoja Jijini Dar es Salaam

Baada ya kupokea taarifa hiyo ambayo imeonyesha zaidi ya Bilioni 13.2 zimetolewa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021. Mhe Makalla alipata wasaa wa kusikia maoni na mawazo kutoka kwa wadau ambao ni wanufaika kama vile makundi maalum ya watu wenye ulemavu, Viongozi wa majukwaa, na muasisi wa VICOBA Bi Devotha Likokola

Aidha RC Makalla ameagiza kufanyika kwa mambo yafuatayo katika Wilaya zote za DSM.

- Mikopo iendelee kutolewa ni takwa la kisheria Mkuu wa Mkoa ameelekeza kuwa Mikopo ya 10% sio hisani ni takwa la kisheria hivyo kila Manispaa ni lazima watekeleze takwa hilo.

- Kufanyika kwa vikao na wadau wa mikopo mara 4 kwa mwaka katika vikao hivyo washirikishwe wadau wote muhimu kama majukwaa anuai ya wanawake, na vikundi vya VICOBA kwa Upande wa Mkoa kwa mwaka vikao vitafanyika mara 2.

- Mafunzo ya masuala ya Fedha wanufaika wa mikopo wapatiwe mafunzo ya masuala ya fedha ili waweze kukopa na kurejesha, kama ni mzalishaji wa bidhaa afundishe namna bora ya kuifanya bidhaa yake iwe na ushindani sokoni.

- Maonyesho ya wanufaika wa mikopo Kila Wilaya iandae Maonyesho ambayo yatatoa ushaidi mzuri kwa mnufaika ili watu wengine waone.

- Maeneo ya kufanyia biashara Kila Wilaya kuwe na maeneo rafiki ya kuwawezesha wanufaika wa mikopo kufanya biashara yenye kuleta tija.

- Mamlaka za Udhibiti biashara* kama TBS na nyinginezo zisiwe kikwazo kwa wafanyabishara ambao ni wanufaika wa mikopo zisiwakatishe taamaa badala yake ziwatie moyo.

- Masoko Wanufaika wa mikopo wakiwa na masoko ya uhakika itasaidia kuwa na uwezo wa kurejesha mikopo yao na namna mojawapo ya kupata masoko ni kuzalisha katika viwango vinavyokidhi ushindani katika Soko hivyo ni jukumu la wataalam kutoa elimu hiyo.

- Majukwaa ya wanawake DSM yafufuliwe maazimio ya kikao majukwaa ya wanawake ambayo yalilenga kuwawezesha Kiuchumi yafufuliwe kwa kuwa ndio sehemu ya wanawake kukutana kujadili biashara na Uchumi.

- Marejesho ya Mikopo RC Makalla amesema mikopo hiyo inatolewa kwa kikundi kwa masharti afanye biashara arejeshe na akopeshwe mwingine hivyo Maafisa maendeleo ya jamii katika kila Wilaya wakasimamie hilo.

Mwisho RC Makalla amesema Rais Samia Suluhu amekuwa akitilia mkazo suala la kuwezesha Kiuchumi makundi maalum, wanawake, na vijana hivyo yeye kama msaidizi wake DSM yuko tayari kutekeleza hilo kwa umakini na weledi mkubwa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa