• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Halmashauri Zichukue Hatua Stahiki kwa wale Wanaohusika na Upotevu wa Fedha za Umma

Posted on: June 22nd, 2023

 

- Apongeza Manispaa ya Temeke na Kigamboni kwa kupata hati safi mwaka wa fedha 2021/2022

-Awataka kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato na kudhibiti matumizi

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Juni 22,2023 amehitimisha ziara yake ya kushiriki *vikao vya kikanuni vya mabaraza ya kupitia hoja za CAG katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke na Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

RC Chalamila amezitaka Halmashauri hizo kupitia Wakurugenzi wake kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wanaohusika na upotevu wa fedha za umma.

Ameyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati wa vikao hivyo katika *Manispaa ya Temeke na kuhitimisha Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni

RC Chalamila amepongeza Manispaa hizo kwa kupata hati safi kufuatia ripoti ya mdhibiti na mkaguzi wa Hesabu za Serikali CAG ya mwaka wa fedha 2021/2022 vilevile Ofisi ya CAG kupitia Ukaguzi wa Hesabu uliofanywa uliopekelea kubaini kasoro mbalimbali ambazo zinafanyiwa kazi na Halmashauri kwa masilahi mapana ya Umma

Aidha Mhe Chalamila amesema lazima Halmashauri zisimamie vizuri ukusanyaji wa mapato na kudhibiti matumizi ya fedha katika maeneo yao, pia kufanya kaguzi za mara kwa mara, kuongeza juhudi katika kuzuia hoja za CAG, usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo, manunuzi ya Umma, kuhakikisha Mikopo iliyotolewa ya asilimia 10 inarejeshwa, kuboresha masoko ili kuongeza mapato na kuitumia vizuri Ofisi ya mkaguzi wa ndani

Hata hivyo RC Chalamila amewataka madiwani kuwaelimisha wananchi kuhusiana na mkataba wa uendelezaji na Ubia wa Bandari ya Dar es Salaam kwa kuonyesha tija ya mkataba huo kwa umma na dhamira ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili kuepuka upotoshwaji unaofanywa na watu wasioitakia mema nchi ya Tanzania

Sambamba na hilo Mhe Chalamila amesema anatarajia kufanya ziara katika Wilaya zote za mkoa huo kwa lengo la kutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa na kusikiliza kero za wananchi

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa