• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Atembelea na Kukagua Miradi Mbalimbali ya Maendeleo Jimbo la Kibamba Ubungo

Posted on: April 9th, 2025

-Amshukuru Rais Dkt Samia  kwa kutoa pesa nyingi zinazowezesha utekelezaji wa miradi hiyo
-Ataka usimamizi mzuri wa miradi kwa kuzingatia viwango na thamani ya pesa
-Asikiliza kero za wananchi wa Kata ya Saranga na kuzipatia majibu papo hapo


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila leo April 09,2025 amefanya ziara ya kutembelea ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Kibamba wilaya ya Ubungo na kuagiza miradi hiyo kujengwa kwa viwango na kuzingatia thamani ya fedha, ambapo ameagiza miradi hiyo kukamilika kwa wakati


Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa jengo la mama na mtoto kwenye kituo cha afya cha Mpiji Magoe RC Chalamila amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa pesa nyingi ambazo zinawezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo ambapo amesema ni muhimu kufanya ujenzi wa miradi unaozingatia thamani ya fedha, miradi inayoweza kudumu kwa miaka mingi na ujenzi ukamilike kwa wakati ili kumaliza adha kwa akina mama na watoto
Akiwa kwenye mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari Goba Kulangwa RC Chalamila amesisitiza suala la ulinzi na usalama hasa nchi ikiwa inaelekea kwenye uchaguzi mkuu hivyo ameagiza kukamilishwa kwa ujenzi wa kituo cha polisi cha Tegeta A


Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo Juma Japhari Nyaigesha amewataka wananchi na wafanyabiashara kuto kukwepa kulipa kodi kwani ndio chanzo cha kupata fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo vituo vya afya huku Mganga Mfawidhi wa kituo cha Afya Mpiji Magoe Hereswida Cosmas akieleza maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo la mama na mtoto amesema ujenzi unaendelea vizuri na utakamilika kwa wakati.


Aidha Katika ziara hiyo wilayani Ubungo RC Chalamila pia ametembelea na kukagua mradi wa maji wa kibamba, pamoja na kukagua mradi wa shule ya sekondari goba kulangwa

Mwisho RC Chalamila amefanya mkutano wa hadhara Kata ya Saranga eneo la ofisi ya Serikali ya mtaa na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi ikiwemo ubovu wa barabara, changamoto ya TASAF, Maji, kusuasua kukamilika kwa ujenzi wa zahanati ambapo ameahidi kabla ya kufika ijumaa ya wiki ijayo pesa tasilimu shilingi milioni 100 zitakuwa zimeletwa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Zahanati hiyo hata hivyo ametolea ufafanuzi kero zingine kwa kuwahakikishia Rais Samia yuko kazini Changamoto zote zitatuliwa

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa