• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Ataka Watendaji wa Kata na Mitaa kuwa Waadilifu

Posted on: November 23rd, 2023

 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila amewataka watendaji wa kata na mitaa kuwa waadilifu wakati wote wanapotekeleza majukumu yao kwa kuwa wanaishi na jamii moja kwa moja vile vile miradi mingi ya mendeleo inatekelelezwa katika ngazi ya Kata au mtaa

RC Chalamila ameyasema hayo leo Novemba 23, 2023 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maafisa Tarafa na watendaji wa kata wa mkoa wa Dar es salaam uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke yatakayofanyika kwa siku mbili kuanzia leo na kesho Novemba 24,2023.

Vilevile amesema watumishi wanapaswa kuwa na maadili ili kuleta  picha nzuri kwa wananchi ikiwa wakiharibu lawama za wananchi zinaenda moja kwa moja kwa viongozi wa juu.

Aidha Mhe. Chalamila amewataka watumishi hao waelewe uadilifu si umaskini na utajiri si wizi, "Kuna utofauti mkubwa kati ya uadilifu na umaskini na wengi wanadhani muadilifu ni kuwa maskini, kwahiyo acheni kuishi kimaskini ili muonekane ni waadilifu."

Pia RC Chalamila amesema mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa sana na aliwaasa viongozi hao kutatua kero na changamoto za wananchi ikiwemo migogoro ya ardhi, kusimamia amani na usalama wao, usimamizi mzuri wa miradi na pesa wanazokabidhiwa zitumike kama zilivyopangiwa, wajiepushe na vitendo vya rushwa na kuwadhulumu wanyonge haki zao.

Naye Mkuu wa wilaya ya Temeke Mhe Sixtus Mapunda alisema mafunzo ni mama wa uelewa wa mambo yote na kuhimiza yawe yanatolewa mara kwa mara ili kuzidi kuwajengea uwezo na kutambua nafasi zao kama watumishi sababu wao ndiyo wapo karibu zaidi na wananchi na kutambua kero na changamoto zao.

Kwa upande wa mwenyekiti wa mafunzo hayo Hulda J. Ulomi alitoa neno la shukrani kwa Mhe Chalamila kwa kufunguzi na maelezo yake, na kuahidi kwamba watafuatilia mafunzo yote kwa umakini na kwenda kuwa bora zaidi katika utendaji wa majukumu yao

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa