• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Aongoza Kikao cha Baraza la Biashara-DSM

Posted on: January 22nd, 2025

 

-Amshukuru Rais Dkt Samia kwa kuendelea kuboresha mazingira ya wafanyabiashara.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila leo Januari 22, 2025 ameongoza kikao cha Baraza la Biashara Mkoa wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Hotel ya Four Points Posta Ilala.

RC Chalamila wakati anafungua kikao hicho amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara hapa nchini hususani Mkoa wa Dar es Salaam " Mhe Rais ameunda timu ya watalaam wabobevu kupitia masuala ya kikodi kwa lengo la kuja na suluhu ya malalamiko ya wafanyabiashara kuhusu kodi kandamizi hii ni ishara ya dhamira njema ya Mhe Rais" Alisema RC Chalamila

RC Chalamila kupitia kikao hicho alitoa nafasi kwa wafanyabiashara kueleza changamoto na vikwazo vya kibiashara, ushauri, maoni pamoja na mapendekezo yao vilevile ufafanuzi wa maeneo ambayo yalikuwa yakilalamikiwa siku za nyuma kama yamefanyiwa kazi au la!

Aidha RC Chalamila amewahakikishia wafanyabiashara kuwa Mkoa utaendelea kuweka mipango ya maendeleo ya kibiashara kupitia maoni na ushauri unaotolewa katika vikao vya mabaraza ya Biashara Mkoa pia amewataka kutumia vizuri fursa zilizoko ikiwemo kufanya biashara saa 24 pamoja na fursa za Uchumi wa bluu.

Kwa upande wa Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Toba Nguvila amesema kikao hicho ni muhimu  kwa masilahi mapana ya maendeleo ya Biashara katika kukuza uchumi  wa Mkoa na Taifa hivyo ameahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa pia kuhakikisha vikao hivyo vinafanyika kama inavyoelekezwa kwa mujibu wa sheria katika ngazi ya Mkoa na wilaya zote tano.

Naye mwenyekiti wa Baraza la wafanyabiashara Mkoa Bwana Denis Chacha ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo kutoa ushirikiano kwa Serikali ili kuzipatia ufumbuzi changamoto zao ambapo amesema watafanya kikao chao ili kutoa fursa zaidi za kueleza changamoto zao

Mwisho kikao hicho kimehudhuriwa na wafanyabiashara, wawekezaji, watalaam wa kutoka Wizara ya biashara, Sekretariati ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na makatibu Tawala wa Wilaya zote za Mkoa





Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa