• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RAS MADENGE ASISITIZA UTOAJI HUDUMA BORA ZA AFYA KWA WANANCHI

Posted on: January 24th, 2023

- Akemea tabia ya baadhi ya watumishi wa afya wenye lugha Zisizoridhisha kwa Wananchi.

- Atoa Wito kwa Wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo ya Surua kuanzia February 01 hadi February 05.

- Mganga Mkuu DSM Ataka Maandalizi ya Utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote.

Viongozi na wasimamizi wa Sekta ya Afya Mkoa wa Dar es salaam Leo wamekutana kwenye kikao kazi Cha kuweka mikakati madhubuti ya maboresho ya utoaji wa huduma Bora za Afya na Maandalizi ya Utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote pindi muswada utakapopitishwa.

Akifungu Kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam Bi. Rehema Madenge ametoa wito kwa watumishi wa afya kuhakikisha wanatoa huduma Bora na zenye ufanisi kwa Wananchi Ili kuondosha Hali ya malalamiko.

Aidha Bi. Madenge Amekemea tabia ya baadhi ya watumishi wa afya wenye lugha Zisizoridhisha kwa Wananchi wanaokwenda kupata huduma huku akipongeza watoa huduma za Afya Mkoani humo kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya.

Katika hatua nyingine RAS. Madenge ametoa wito kwa Wazazi ambao watoto wao hawakupata chanjo ya Surua kuwapeleka kupata chanjo hiyo inayotaraji kutolewa February 01 hadi February 05 mwaka huu.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dr. Rashid Mfaume amewaelekeza Waganga wafawidhi wa Vituo vya Afya kuanza Maandalizi ya kupokea na kutekeleza Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote pindi muswada utakapopitishwa kwa kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakuwa zenye ubora.

Pamoja na hayo Dr. Mfaume amesema takwimu zinaonyesha kati ya *Wananchi 100 ni Wananchi 15 pekee ndio wenye bima ya Afya jambo ambalo linawalazimu kuendelea kutoa Elimu ya umuhimu wa Bima ya Afya.

Kikao hicho kilichojumiisha waganga wakuu wa Wilaya, Makatibu wa Afya na Waganga wafawidhi kutoka Vituo 142 vya Afya Mkoani humo kimetoa fursa pia ya kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuboresha utendaji kazi

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA AFUNGUA MKUTANO WA "AFRICA E- MOBILITY FORUM"

    March 21, 2023
  • RC Makalla Akabidhi Hundi ya Mikopo ya 10% zaidi ya Bilioni 4.6 Temeke Atoa Maagizo Matano

    March 20, 2023
  • RC Makalla Masoko Mapya Yatakayojengwa Washirikishwe Machinga na Viongozi wa Soko

    March 11, 2023
  • RC Makalla Aeleza Kishindo Cha Rais Dkt Samia Suluhu Miaka 2 DSM

    March 10, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akikagua Maendeleo ya Ujenzi na ukarabati wa Soko la Kariakoo
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa