• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

MAMA JANETH MAGUFULI : "MASHIRIKA YA UMMA, SEKTA BINAFSI SHIRIKIANENI NA SERIKALI KATIKA KUMUWEZESHA MWANAMKE”

Posted on: March 8th, 2018

Mashirika ya Umma na Sekta binafsi kote nchini yametakiwa kuhakikisha yanashirikiana bega kwa bega na Serikali katika kumuwezesha mwanamke kujikwamua kiuchumi na kimaendeleo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mama Janet Magufuli, Mke wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania alipokuwa Mgeni rasmi siku ya maadhimisho ya mwanamke duniani yenye kauli mbiu isemayo "Kuelekea Uchumi wa viwanda tuimarishe usawa wa Jinsia na uwezeshaji wa wanawake vijijini."

Amesema kufuatia kauli mbiu hiyo wanawake wanatakiwa kujengewa uwezo ikiwemo elimu ya ujasiriamali, mafunzo, ili kupata mbinu za kuwekeza, mitaji pamoja na maeneo kwa lengo la kumsaidia mwanamke kujikwamua kiuchumi.

Ameongeza kuwa lengo la siku ya wanawake duniani ni kutukumbusha harakati na mafanikio yaliyokwisha fanyika katika kumkwamua mwanamke dhidi ya unyanyasaji, hali duni, kutelekezwa na kuhakikisha haki yake inapatikana, inaheshimiwa na kuenziwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar Es salaam Mh Paul Makonda alipotoa nasaha zake wakati wa maadhimisho hayo amesema wanawake wa Mkoa wa Dar Es Salaam wanajitahidi Sana katika kuhakikisha wanaendana na kasi iliyopo ya uchumi wa viwanda.

Amebainisha kuwa katika Mkoa wake kunajumla ya vicoba 2748 vyenye mtaji wa takribani bilioni 10.78 ambavyo vinaendeshwa na wanawake.

Aidha amebainisha kuwa katika mkoa wake unajumla ya idadi ya watu milioni 6, na kati ya hao wanawake ni wengi kuliko wanaume, hivyo ni jeshi kubwa ambalo likiwezeshwa linaweza.

Maadhimisho haya ya siku ya wanawake yaliyofanyika kimkoa katika Manispaa ya Ubungo katika ukumbi wa Mlimani city yalihudhuriwa na viongozi wa Vyama na Serikali,pamoja na vikundi mbalimbali vya wajasiriamali kutoka Manispaa ya Kinondoni, Ilala, Temeke, Kigamboni na Ubungo.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa