• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Dkt Hussein Ally Mwinyi Aweka Jiwe la Msingi Barabara ya Kiibada, Mwasonga-Kimbiji

Posted on: April 25th, 2025

 

-Ikiwa ni Shamra Shamra kuelekea maadhimisho ya miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt Hussein Ally Mwinyi ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya kibada mwasonga hadi kimbiji yenye kilometa 41 na kuagiza ikamilike kwa wakati na kwa viwango huku akisisitiza suala la amani ya Nchi kwani ndio msingi wa kuimarika kwa miradi yote

Akizungumza leo April 25,2025 Wilaya Kigamboni Jijini Dar es salaam katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya kibada-Mwasonga hadi kimbiji kwa kiwango cha lami Rais Dkt Hussen Mwinyi amesema uwepo wa amani ndio jambo lililowezesha ujenzi wa barabara hiyo ya kibada na zingine nyingi hivyo ni muhimu kuendelea kudumisha amani ambapo ameagiza ikamilike kwa wakati na kwa ubora.

Akizungumzia suala la muungano Dkt Mwinyi amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuendelea kudumisha muungano na kuendelea kumaliza kero za muungano jambo ambalo limezidi kuimarisha umoja

Awali kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar kuongea akiongea kwa niaba ya waziri wa ujenzi Waziri wa Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari Jerry Silaa amesema barabara hiyo imekuwa ni kilio cha muda mrefu cha wananchi na sasa kwa ujenzi huo inakwenda kuifungua kigambani kiuchumi kwa kuwezesha wawekezaji kufanya kazi kwa ufanisi

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila amemhakikishia Rais wa Zanzibar kuwa Mkoa upo salama na utaendelea kuwa salama licha ya uwepo vuguvugu la kisiasa huku akimppngeza Rais Dkt Samia kwa kuwezesha barabara hiyo kujengwa pamoja na kuwezesha miradi muhimu ikiwemo ya umeme sanjari na kumpongeza Rais Mwinyi kwa kuboresha miundombinu na miradi mbalimbali ya maendeleo Zanzibar

Aidha Akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo yenye jumla ya kilometa 41 Mtendaji mkuu wa TANROAD Mhandisi Muhammed Besta amesema ujenzi wa barabara hiyo umegawanywa kwenye vipande viwili ukigharimu kiasi cha shilingi bilioni 83.8 chini ya mkandarasi wa kampuni ya Estim na tayari ujenzi hadi sasa umefikia asilimia 30

Mwisho uzinduzi huo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya kaulimbiu isemayo ''Muungano wetu,heshima na tunu ya Taifa' shiriki uchaguzi mkuu wa mqaka 2025

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa