• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

CCM-DSM Yaridhishwa Namna TARURA Inavyotekeleza Miradi ya Barabara

Posted on: November 27th, 2023

 

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam leo Novemba 27,2023 imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya barabara inavyotekeleza na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini TARURA katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo ikiwemo Barabara ya Kinzudi- Goba Wilaya ya Ubungo, Jamirex-Mwenge Wilaya ya Kinondoni na Chanika Homboza Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam.


Akiongea wakati wa ziara hiyo kwa niaba ya CCM Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa Mhe Abbas Mtevu amesema Chama kimeridhishwa namna Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini TARURA inavyotekeleza ujenzi wa miundombinu ya Barabara katika Mkoa huo ambapo ametoa maelekezo kwa TARURA kujipanga vizuri katika ukarabati wa barabara pindi zinapokuwa na mashimo na kuzikarabati mapema kabla hazijaharibika zaidi.

Kwa Upande wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amesema maeneo ambayo yana Changamoto kubwa za Barabara katika Mkoa huo ni Wilaya ya Ubungo na Kigamboni lakini Mhe Rais Dkt Samia tayari ameshaidhinisha pesa kupitia DMDP awamu ya pili ambazo zinakwenda kupunguza Changamoto za Barabara kwa kiwango kikubwa katika Wilaya hizo.

Aidha Mhe Albert Chalamila amesema katika kukabiliana na uharibifu wa miundombinu unaotokana na mvua zinazoendelea kunyesha tayari Mkoa umejipanga kujenga miundombinu hiyo mara tu mvua zikiisha ili kuepuka hasara zisizo za lazima labda tu kwa eneo ambalo litaonekana kuwa na ulazima nyakati za mvua Mkoa utafanya hivyo " Vilevile Ujenzi utakofanyika sasa lazima uakisi mabadiliko ya tabia ya nchi" Alisema RC Chalamila.

Naye Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini TARURA Mkoa huo Mhandisi Godfrey Mkinga amesema TARURA inasimamia Mtandao wa Barabara wenye jumla ya urefu wa Kilometa 5,059.05, mtandao umegawanyika katika sehemu kuu tatu, Barabara za Mlisho (feedders), Barabara za Mkusanyo (Collector) na Barabara za Jamii (Community) ambapo amesema kati ya hizo urefu wa Kilometa 610.69 ni barabara za Lami/Zege, Kilometa 1,642.90 ni barabara za changarawe, na Kilometa 2,805.48 ni barabara za udongo

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa