• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Ilala MC
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

UBALOZI WA CHINA WAMZAWADIA RC MAKONDA MAJENGO MATANO YA KISASA YA OFISI ZA WALIMU DAR

Posted on: February 15th, 2018

Ubalozi wa China Nchini Tanzania umeguswa na kazi nzuri inayofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kuboresha mazingira ya walimu na kuamua kumzawadia Majengo Matano ya kisasa kwa ajili ya ofisi za walimu ambapo leo RC Makonda ameweka jiwe la Msingi kuashiria kuanza kwa Ujenzi huo kwenye Shule ya Sekondari Makumbusho pamoja na kukabidhi Ramani ya Majengo.

Ujenzi wa Majengo hayo Matano ni matokeo ya RC Makonda kuwasilisha ombi la ujenzi wa ofisi za walimu kwa Balozi wa China nchini Tanzania na kwa kuwa kazi anayofanya RC Makonda inaonekana Balozi huyo alipokea kwa mikono miwili ombi hilo.

Majengo hayo yatajengwa kwenye Wilaya Tano za Mkoa wa Dar es salaam ambapo ndani yake zitakuwa na Ofisi ya Mwalimu Mkuu, Mwalimu mkuu msaidizi, Ofisi ya walimu wote, ukumbi wa mikutano, chumba cha kuhifadhi mitihani, vifaa vya michezo, chumba cha muhasibu, chumba cha kubadili nguo, mapokezi, vyoo, bafu huku zikisheheni furniture za kutosha ikiwemo viti, meza, makabati na AC ambapo ujenzi wa jengo hilo unataraji kukamilika ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa.

RC Makonda amemshukuru Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke kwa ujenzi wa majengo hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yanaenda kupunguza mateso ya walimu kufanya kazi katika mazingira magumu ikiwemo kufanya kazi kwenye madarasa.

Amesema dhamira yake katika kuboresha mazingira ya walimu ni kuwawezesha kutoa elimu bora itakayowezesha Taifa kuwa na wataalamu wa kutosha.

Kwa upande wake Balozi wa China Nchini Tanzania Bi. Wang Ke amesema kwa miezi mitatu aliyoishi hapa nchini tangu alipoteuliwa kuwa balozi ameshuhudia maendeleo makubwa aliyofanya RC Makonda hivyo wameona wasikae kimya kwenye jambo hilo linalolenga kuleta ukombozi wa uchumi kupitia elimu.

Nao walimu wa shule ya makumbusho wamemueleza RC Makonda kuwa awali walikuwa wakitumia madarasa manne ya wanafunzi hivyo ujenzi wa jengo hilo ni neema kwao kwa kuwa madarasa hayo yatarejeshwa kwa wanafunzi.

TUSHIRIKIANE KWA PAMOJA KUBORESHA MAZINGIRA YA ELIMU KWA MANUFAA WATOTO WETU.

Matangazo

  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Serikali - AWAMU YA PILI January 08, 2021
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge: Stendi Mpya ya Mabasi ya Mbezi Louis Kuanza Rasmi Novemba 30, Majaribio Novemba 25

    November 09, 2020
  • RC Kunenge Afanya Ziara ya Kushtukiza Usiku wa Manane,Atoa Maagizo Mazito kwa Wakandarasi "Wazembe'

    October 17, 2020
  • Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Akutana na Walimu,Awahakikishia kuwa Serikali Itaendelea Kulipa Malimbikizo Yote Wanayodai

    September 22, 2020
  • RC Kunenge Atembelea Miradi na Kutaka Ikamilike kwaWakati

    September 17, 2020
  • Tazama zote

Video

Kampeni ya Tahadhari Dhidi ya Mafuriko kwa Wanafunzi jijini Dar es Salaam
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa