Kuratibu masuala yote ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Kuratibu Mipango na Bajeti ikiwemo Mpango Mkakati na Mipango kazi.
Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa mkataba wa huduma kwa wateja.
Sekretarieti katika vikao vya Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC).
Kuunganisha, kuratibu na kufuatilia Mipango na Bajeti za Serikali za mitaa.
Kutoa huduma za kitaalam katika utekelezaji wa Mfumo wa habari na mawasiliano.
Kuratibu miradi ya Wahisani mkoani
Kumshauri Katibu Tawala wa Mkoa juu ya masuala ya mashirika ya Umma, mashirika yasiyo ya kiserikali na sekta binafsi
Kuratibu shughuli za utafiti mkoani
Kuratibu zoezi la Sensa.
Kuziwezesha mamlaka za Serikali za mitaa juu ya utekelezaji wa sheria ya mazingira Na. 2 ya 2004.
Kumshauri Katibu Tawala wa Mkoa na Halmashauri juu ya utekelezaji wa sheria za kazi.
Kuratibu masuala ya Maafa katika mkoa.
|