JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
     

KILIMO

 
Kilimo [ Mifugo ] [ Nyumbani ] au
 
 
Utangulizi
 

Kilimo ni Sekta muhimu kwa maisha na uchumi wa wakazi wa Mjini na pembezoni mwa Mji.

 
 
Eneo linalofaa kwa kilimo na ufugaji ni hekta 107,500, ambapo Manispaa ya Temeke ni hekta 55,000, Kinondoni hekta 37,000 na Ilala hekta 15,000. Hadi sasa eneo linalotumika kwa kilimo ni Ha.32,972 sawa na asilimia 31 ya eneo lote. Hali hii inatokana na maeneo ya mashamba kutwaliwa kwa ajili ya kupimwa viwanja vya makazi na wawekezaji.
 
 

Mazao makuu yanayolimwa ni mihogo, viazi vitamu, mpunga, mahindi, migomba na kunde. Mazao ya biashara ni korosho, minazi, mboga, matunda, maua na viungo. Mkoa utoa kipaumbele katika kilimo cha mboga matunda na viungo (high value crops) ambayo yana soko la uhakika hapa Jijini.

 

 

 
 

Kilimo cha Mjini (Mboga na matunda) huchangia lishe bora, mapato na uboreshaji mazingira Jijini.

 

 

 

Msimu wa 2008/2009 lengo lilikuwa kununua tani 3,500 za korosho. Soko la korosho lilifunguliwa mwezi Oktoba na bei ya T.shs. 675 daraja la kwanza std. Na T.shs. 540 daraja la pili na ilitangazwa. Hali ya ununuzi ni mbaya, kwani Makampuni yaliyochukua leseni kununua korosho yamegoma kwa madai ya bei kubwa.

 
 
Kilimo cha Mbogamboga

Kilimo cha Mbogamboga

 
 
Kilimo cha Maua
Kilimo cha maua
 
Kilimo cha Korosho
 

Kwa mahitaji ya chakula Mkoa huzalisha asilimia 17 hadi 20 ya mahitaji ya chakula ambayo ni tani 1,053,000 kwa mwaka. Aidha asilimia 80 hadi 83 ya mahitaji ya chakula hutoka Mikoa mingine na nje ya Nchi

 
 
Korosho ni zao kuu la biashara mwaka 2007/2008 Mkoa uliuza jumla tani 3,338.5 za korosho ghafi zenye thamani ya T.shs. 1,633,593,908. Chama Kikuu cha Ushirika DARECU na Vyama vya Msingi vya Ushirika vilihusika katika ununuzi wa korosho.
 
 

Msimu wa 2008/2009 lengo lilikuwa kununua tani 3,500 za korosho. Soko la korosho lilifunguliwa mwezi Oktoba na bei ya T.shs. 675 daraja la kwanza std. Na T.shs. 540 daraja la pili na ilitangazwa. Hali ya ununuzi ni mbaya, kwani Makampuni yaliyochukua leseni kununua korosho yamegoma kwa madai ya bei kubwa.

Utekelezaji Miradi ya DADPs

 

Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam zimekwishapata jumla T.sh 418,822,889/= robo ya kwanza na ya pili kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kilimo.
 
 
Katika kipindi cha Julai hadi Oktoba shughuli zilizofanyika ni kukamilisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya mwaka 2007/2008. Fedha zilizotolewa robo ya kwanza na ya pili, mchakato wa kuzipeleka kwa walengwa unaendelea.
 
     
     
 
Kilimo [ Mifugo ] [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2007 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, TEL: 022 - 2203156/2203158, FAX: 022-2203158