JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
     
Kituo cha Mabasi Ubungo
 
Kituo cha Mabasi Ubungo [ Nyumbani ] au
 

Utangulizi

 
 

Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo(Ubungo Bus Terminal) hutoa huduma za usafiri kwa magari yaendayo mikoani na nchi jirani; kilianzishwa na iliyokuwa Tume ya Jiji la Dar es Salaam na kilifunguliwa rasmi na Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 6/12/1999.

Madhumuni ya kuanzisha kituo ni kama ifuatayo:

 

  • Kutoa huduma bora kwa wasafiri na watumiaji wengine.
  • Kuondoa msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dar es Salaam uliosababishwa na mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani kuegeshwa katika barabara za Msimbazi, Bibi Titi Mohamed (Mnazi Mmoja) na Morogoro (Eneo la Kisutu).
  • Kuongeza mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kituo hiki kina ukumbwa wa Hekta 8.2. Kina uwezo wa kuhudumia wastani wa mabasi makubwa 350, madogo 70, wasafiri, wasindikizaji pamoja na watoa huduma mbalimbali kituoni wasiopungua 30,000 kwa siku. Sambamba na huduma za usafiri zipo pia huduma za kiuchumi zinazoendeshwa na Sekta binafsi, mfano Hoteli, maduka, karakana, kituo cha mafuta n.k.

 
Tangu kuanzishwa kwake Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imekuwa ikifanya juhudi za kuboresha huduma, kuongeza usalama wa wasafiri na mali zao, na mapato kwa Halmashauri.
 
 
 
 

Kutokana na mahitaji ya huduma ya wasafiri kuongezeka, Halmashauri ya Jiji imepanga kupanua huduma za kituo hicho ili kiwe cha kisasa na kuendelea kutoa huduma bora zaidi. Umeandaliwa mpango wa biashara, (Business Plan) ambapo LAPF wataingia ubia na Halmashauri ya Jiji ili kuupanua mradi huo kwa kuanzia mwaka huu wa fedha 2008/09. Baadhi ya upanuzi utakaofanywa ni kujenga majengo marefu ya biashara zikijumuisha biashara ndogo ndogo, za kati na za daraja la juu, kuongeza huduma za mahoteli, vyumba vya malazi, ofisi mbalimbali na vituo vingine muhimu kama vya kubadili fedha n.k.

 

 
 
 
 
Picha ikionyesha jengo la kupandia/kushukia kwenye basi kama litakavyoonekana (baada ya kuboreshwa) kutokea Chuo Kikuu cha DSM na majengo mengine ukianzia na Hoteli, Jengo la Kungojelea na kupaki magari, jengo la maduka na ofisi, na jengo la kukatia tiketi
 
Huduma mbalimbali zitolewazo kituoni hapo:
 
 
Kituo kinatoa ajira kwa zaidi ya watu 1,000 na huduma zilizopo huwaleta zaidi ya watu 30,000 kwenye kituo kwa siku. Vilevile kimevutia wawekezaji hasa wa mahoteli na majengo ya ofisi jirani na kituo, hususani maeneo ya Sinza, Manzese na Ubungo yenyewe.
 
Kituo kina jumla ya Migahawa/bar 25 ambayo hutoa huduma kwa wasafiri na watu mbali kituoni hapo na maeneo jirani.
Kituo kina jumla ya maduka/vibanda 106 ambayo hutoa huduma kwa wasafiri na jamii inayoizunguka.
Hali ya usafi

Usafi wa maeneo yote ya wazi ya Kituo unafanywa na Mkandarasi AJM Rafiki wa Mazingira. Mkandarasi huyu anasimamiwa ipasavyo ili kuhakikisha Kituo kinakuwa safi.

 
 
Mazingira ya Kituo yameboreshwa kwa kupanda miti na kuoteshwa maua sehemu mbalimbali za Kituo.
 
 
Unyunyiziaji wa dawa za kuangamiza wadudu hufanyika kila baada ya miezi mitatu (3) kwenye sehemu mbalimbali za Kituo, kwa ajili ya kuangamiza wadudu mbalimbali.
 
 
Kituo cha Mabasi Ubungo [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2007 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, TEL: 022 - 2203156/2203158, FAX: 022-2203158