JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
     
VVU/UKIMWI
 
Huduma za UKIMWI [ Nyumbani ] au
 
Huduma Za Ukimwi Mkoani Dar es Salaam
 

Huduma za UKIMWI Mkoani Dar Es Salaam zinatolewa katika Manispaa tatu, Temeke Ilala na Kinondoni. Jumla ya vituo 68 vya serikali, 54 vituo binafsi na asasi zisizo za kiserikali (NGOs) zisizopungua mia sita ( 600).

 
 
 
 
Huduma zinazotolewa ni kama zifuatazo:
 
  • Kutoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na huduma endelevu kwa wagonjwa Vituoni
  • Kutoa dawa na huduma endelevu kwa wagonjwa majumbani.
  • Kutoa elimu juu ya ugonjwa na jinsi ya kuzuia maambukizi.
  • Kupunguza maambukizi ya virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTC).
  • Huduma ya kuhakikisha damu salama.
  • Kutoa ushauri nasaha na kupima kwa hiari.
 
 
 

Vituo Vinavyo Pima na Kutoa Ushauri Nasihi.

 

Manispaa

Vituo Vya Serekali

Vituo Binafsi

Mashirika

Asasi

Jumla

ILALA

23

6

7

3

39

KINONDONI

19

11

6

5

41

TEMEKE

26

9

4

3

43

JUMLA

68

26

17

11

123

 

Vituo vya Huduma Na Tiba (Care And Treatment).

 

MANISPAA

VITUO VYA SEREKALI

BINAFSI

JUMLA

ILALA

Amana

Khan

 

 

Mnazi Moja

Aga khan

 

 

Buguruni

St. Bernad

 

 

IDC

Tumaini Hospital

 

 

Tabata A

Regency

 

 

Muhimbili

TMS

 

 

Ocean Road

Hindu Mandal

 

 

 

Buguruni Anglikan

 

JUMLA

 

 

15

KINONDONI

Mwananyamala

TMJ

 

 

Sinza

Mikocheni

 

 

 

Osterbay

 

 

 

IMTU

 

 

 

Massana Hospital

 

 

 

THI

 

 

 

UDSM

 

 

 

Emilio Mzena

 

JUMLA

 

 

10

TEMEKE

Temeke Hospital

T.O.HS

 

 

Mbagala Rangi Tatu

 

 

JUMLA

 

 

4

JUMLA KUU

 

 

29

 

 

Huduma ya Kuzuia Maambukizi Kutoka kwa Mama Kwenda kwa Mtoto.
 

Manispaa ya Ilala vituo 23

Manispaa ya Kinondoni 18.

Manispaa ya Temeke vituo 12

JUMLA Vituo 53.

 
 

 

 
 
 
 
Katikati ni Mganga Mkuu Hospitali ya Mwananyamala akiwa na Wataaalam kutoka Mkoani, walipotembelea Kituo kinachotoa huduma za UKIMWI Hospitalini hapo.
 
 

Katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala huduma hii inatolewa katika kata 19 kati ya kata 22 zilizoko Manispaa ya Ilala kwa kushirikiana na Mashirika yafuatayo:
•  Pathfinder,
•  CCBRT,
•  UMATI,
•   MDH.

 
 

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni huduma inatolewa kwenye kata zote 24 kwa kushirikiana na:
•  UMATI,
•  Action Aid Center ,
•  Pathfinder,
•  Matumaini Counseling Center ,
•  Kimara Peer Educators,
•  PASADA

 
 

Katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke huduma zinatolewa kwenye kata zote 27 kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali yafuatayo;
•  UMATI,
•  PASADA,
•  TOH,
•  Pathfinder, na
•  Vuka Tanzania .

Upimaji wa Virusi vya Ukimwi kwa Hiari.

Katika kipindi cha kampeni ya upimaji virusi vya UKIMWI kwa hiari iliyo zinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete mwezi July 2007, zoezi la kudumu linaendelea katika vituo maalum 6(stand alone VCT Sites) na ndani ya huduma za kawaida za afya kwa utaratibu mpya unaoitwa “Providers Initiated Counseling and Testing”.

 
 

Hali ya Maambukizi.

Taarifa za uchunguzi unaofanywa kila mwaka nchini chini ya usimamizi wa mpango wa kupambana na malaria na UKIMWI (THIMS) inaonyesha kuwa katika mwaka 2008, idadi ya wanaishi na Virusi vya UKIMWI Dar Es Salaam ni wastani wa asilimia 9.3 ukilinganisha na wastani wa kitaifa wa asilimia 5.8. Mkoa wa Dar Es Salaam bado unashika nafasi ya tatu kwa kiwango cha maambukizi ukilinganisha na mikoa mingine kitaifa.

 

Mafanikio.

•  Mkoa wa Dar Es Salaam una zaidi ya NGO Mia sita zinazotoa huduma za UKIMWI na mkoa unashirikiana nao kwa karibu katika kuhakikisha ugonjwa huu unapungua au kutoweka.
•  Kuongezeka kwa vituo vya kupima na utoaji ushauri nasaha katika Manispaa zetu,
•  Kupungua kwa kasi ya maambukizi kutoka 10.9%(Tanzania Health Indicator Survey 2004) na kufikia asilimia 9.3 (KAMPENI 2007).
•  Kuundwa kwa kamati ya TB/HIV ya Mkoa.
•  Upo mpango wa utekelezaji wa TB/HIV ambao unaendelea kuutekeleza kwa ufadhili wa GF kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
•  Mafunzo yametolewa kwa watumishi wa afya wanaoshughulikia huduma za UKIMWI (counsellers).
•  Upatikanaji wa fedha za GF kwenye Manispaa zetu, Temeke ,Ilala na Kinondoni.
•  Lipo gari la Global Fund linalotuwezesha kufanya usimamizi kwa urahisi.
•  Wapo wafadhili wanaowezesha kazi hizi za UKIMWI zifanikiwe mfano MDH, G/F

 
 
Huduma za UKIMWI [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2007 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, TEL: 022 - 2203156/2203158, FAX: 022-2203158