JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
     
Mkakati wa Kilimo kwanza- Dar
 
Uchaguzi Mkuu [ Nyumbani ] au
 
 
 
 

Katika maeneo ya pembezoni mwa Jiji, kilimo ni sehemu kuu ya kupata chakula na mapato. Mazao makuu ya chakula yanayolimwa ni mhogo, viazi vitamu, mpunga, mahindi, migomba na mikunde. Mazao ya biashara ni mikorosho, minazi, na matunda. Aidha, kutokana na uhaba wa ardhi Mkoa unasisitiza kilimo cha mboga matunda na viungo mazao yanayotumia eneo dogo la ardhi na kutoa mapato mengi kwa eka ambayo ni mananasi, machungwa na miembe, mboga na matunda mengineyo. Mazao haya yana soko la uhakika hapa Jijini.

Mahitaji ya chakula kwa mwaka ni tani 1,053,000. Mazao ya chakula yanayozalishwa hapa Mkoani huchangia 17% - 20% ya mahitaji ya chakula kwa mwaka. Aidha, asilimia 80% - 83% ya mahitaji ya chakula hutoka Mikoa mingine na nje ya nchi.

Hali ya kilimo cha pembezoni mwa Jiji bado ni duni ambapo kiwango cha kutumia zana za kilimo ni kidogo na matumizi ya pembejeo za kilimo sio mzuri kutokana na uwezo mdogo wa wakulima. Hata hivyo, hali ya upatikanaji chakula hapa Jijini na vijijini haina tofauti kutokana na wakulima kuhifadhi mazao mashambani kwa mfano mihogo, viazi vitamu na mpunga. Mihogo na viazi vitamu hupandwa nyakati tofauti na kuhifadhiwa ardhini.

Utekelezaji wa mkakati wa kilimo kwanza
Kwa kushirikiana na halmashauri za Mkoa wa Dar es salaam, kilimo kwanza inatekelezwa katika ngazi zote za mkoa na Halmashauri. Ambapo mkoa ulifanya ufuatiliaji na tathimini za utekelezaji. Hata hivyo utekelezaji umefanyika katika maeneo yafuatayo:

• Uhamasishaji na uelimishaji juu ya kilimo bora
Viongozi walihamasisha wananchi kutambua kuwa kilimo ni njia kuu ya kukuza uchumi na kuondoa umaskini.Wataalam 155 wamepangwa katika mitaa yenye kilimo ili ili kuweza kuwahudumia wakulima na wafugaji.Jumla ya vikundi 94 vya wakulima na wafugaji vimepatiwa mafunzo juu ya kilimo bora ili kuzingatia kanuni bora za kilimo na kukifanya kilimo kiwe cha kisasa na chenye kuleta tija kwa wadau wote wa sekta ya kilimo.

Manispaa zote tatu za jiji la Dar es Salaam zinazalisha miche mbalimbali ya miti ya kivuli,matunda,korosho na maua ili kuboresha kilimo mchanganyiko.Aidha Manispaa ya Ilala imekamilisha ujenzi wa darasa katika bustani yake ya Kinyamwezi ambapo wakulima watapatiwa elimu ya kilimo bora pamoja na taarifa za tafiti mbalimbali.
Sheria ndogo ya jiji la Dar es Salaam inayosisitiza ufugaji wa ndani (zero grazing) inatekelezwa.

• Ununuzi wa zana za kilimo( power tillers)
Ununuzi wa power tillers na mafunzo ya matumizi ya power tiller yamefanyika. Utekelezaji wa ununuzi wa power tillers ni kama ulivyoonyeshwa kwenye jedwali lifuatalo:

MANISPAA

KIASI TARAJIWA

KIASI KILICHO NUNULIWA

Temeke

8

2

Ilala

5

3

Kinondoni

8

4

JUMLA

21

9

• Uibuaji wa mipango ya maendeleo ya kilimo/mifugo na samaki
Halmashauri ya manispaa ya Temeke, Ilala na Kinondoni imeibua mipango ya maendeleo kufuatana na mwongozo mpya unaosisitiza kuibua miradi michache yenye tija inayoendana na fungu walilotengewa. Mipango ya maendeleo iko katika hatua za mwisho za ukamilishaji ili itumwe Tamisemi kwa uchambuzi zaidi.

Utekelezaji Malengo ya Kilimo
Katika msimu wa kilimo 2005/2006 hadi 2009/2010 lengo na utekelezaji halikufikiwa kama ilivyopangwa kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na tabia nchi, hii ilisababisha hali ya ukame na mvua zisizoendana na misimu ya kilimo (mtawanyiko mbaya ).

 

 

 

 
 

Kilimo Cha Umwagiliaji
Kilimo cha umwagiliaji kinatekelezwa katika mabonde kwa kutengeneza majaluba ya kuvuna maji ya mvua kutumia Mito iliyopo na kuchimba visima virefu na vifupi.Mkoa umeainisha maeneo maalum yatakayotumika kwa Kilimo cha Umwagiliaji.Aidha, kwa kupitia program ya ASDP Mkoa unatarajia kuomba fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya umwagiliaji katika maeneo yafuatayo:
Manispaa ya Temeke: Kata ya Pemba Mnazi hekta 4000,Kisarawe II hekta 150,Kimbiji hekta 102,Somangila hekta 100 na Chamazi hekta 20.
Manispaa ya Ilala :Kata ya Chanika hekta 3400, Kata ya Msongola 1600.
Hii inafanya Mkoa kuwa na jumla ya hekta 10,156 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji.Maeneo yatakayolima Mpunga yatatumika pia katika kulima mazao kama Matikiti maji, Matango,viungo, mahindi mabichi na viazi vitamu mara baada ya kuvuna mpunga,Mazao haya huchukua muda mfupi kukomaa hivyo kusaidia kuingiza mapato katika muda mfupi.

Hali ya Chakula:
Mkoa wa Dar es Salaam kwa ujumla hauna upungufu wa chakula kwa sababu asilimia 83% ya chakula inatoka nje ya Mkoa. Mkoa wenyewe unachangia 17% - 20% ya mahitaji ya chakula kwa mwaka kama tulivyoeleza hapo awali.Tatizo ni kupanda kwa bei za vyakula wakati mapato ya walio wengi yako chini.

Taarifa ya bei za mazao kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2005 hadi 2010
Kwa wastani wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanaweza kuwa na upatikanaji hafifu wa chakula kuanzia mwezi Machi hadi Juni miezi ambayo kunakuwa na upungufu wa chakula Mikoani. Katika kipindi hiki wananchi walioko pembezoni mwa mji hutegemea akiba ya mazao kama mihogo,viazi vitamu vinavyolimwa mabodeni, mboga na matunda ambayo haijavunwa mashambani.

Miradi ya DADPS
Kwa kipindi cha mwaka 2006/2007 hadi 2009/2010 jumla ya miradi 14 ya DADPs imekuwa ikitekelezwa.

 

Miradi iliyokuwa ya maendeleo ya kilimo kwa kipindi cha mwaka 2006/2007 hadi 2009/2010 ni kama ilifuatavyo; • Kuongeza matumizi ya wanyama kazi kwa kununua majembe ya kukokotwa na ng'ombe
• Uboreshaji wa miundo mbinu ya umwagiliaji
• Uboreshaji wa miundo mbinu ya mifugo (josho, machinjio na uhamilishaji)
• Mradi wa ng'ombe na mbuzi wa maziwa
•Uendelezaji wa zao la korosho
•Mafunzo kwa watumishi na wakulima
• Ujenzi wa shade ya kuuzia matunda
• Usambazaji wa miche bora ya matunda, maua, mikorosho na miti ya kivuli
• Udhibiti wa magonjwa ya wanyama na mimea
• Uboreshaji wa huduma za ugani
• Ununuzi wa matrekta madogo (Power tillers)
• Uongezaji thamani ya mazao ya chakula na biashara (usindikaji zao la muhogo na mbegu za mafuta)
•  Uboreshaji wa kuku wa kienyeji
•  Uzalishaji wa mazao yasiyo ya asili (uyoga)

Miradi ya maendeleo ya kilimo imekuwa na manufaa kwa wadau wa sekta ya kilimo kwa;
• Kipato kimeongezeka
• Afya zimeboreka kwa kupata lishe bora
•  Eneo la uzalishaji pamoja na mazao limeongezeka
•  Ongezeko la wanachama wanaonufaika na miradi
• Ongezeko la ajira.

 

 

 

 

 

Soma zaidi kuhusu Nguzo Kumi za Utekelezaji wa Kilimo Kwanza

 

 

 
 
 
 
 
 
Uchaguzi Mkuu [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2007 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, TEL: 022 - 2203156/2203158, FAX: 022-2203213