Siku hii huadhimishwa kwa lengo la kukumbuka mauaji ya kinyama waliofanyiwa watoto nchini Afrika ya Kusini wakati wakidai haki zao za msingi, pia kuwakumbusha wazazi/walezi na jamii kwa ujumla juu ya haki na wajibu wa jamii katika kuwalea watoto. Aidha, hutoa nafasi ya kuwakumbusha watoto haki na wajibu wao kama watoto katika Taifa |