Huduma za kibenki katika Mkoa wa Dar es Salaam ni za kutosha na uhakika. Makao Makuu ya Benki Kuu ya Tanzania(BoT) yapo Jijini Dar es Salaam, zipo Benki za Biashara, Maduka ya Kubadilisha Fedha za kigeni (Foreign Exchange Bureau), Makampuni ya Bima (Insurance Companies). Baadhi ya benki za biashara ni kama vile:NBC, NMB, CRDB, Postal Bank, Barclays, Standard Chartered (T) Limited, Kenya Commercial, Akiba, Stanbic, Exim, Citibank, FBME Bank, Euro African, Diamond Trust, International Commercial Bank, Habib African Bank, African Banking Corporation, United Bank of Africa, CF Union Bank Savings and Finance Commerce Bank, Azania Bancorp, TIB, Twiga Bancorp Limited, Baroda na Dar es Salaam Community Bank ambayo inamilikiwa kwa pamoja na Halmashauri ya Jiji na Halmashauri za Temeke, Kinondoni na Ilala.
|