Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 Mkoa wa Dar es Salam ulikuwa na idadi ya watu wapatao 2,487,288 ambao wanaishi kwenye mitaa ipatayo 387. Idadi hii ya watu inapata huduma za afya kinga na tiba kupitia vituo vya kutolea huduma vya Serikali, Mashirika ya dini na yasiyo ya Kiserikali na Sekta binafsi. Kuna jumla ya Hospitali 27 ambapo za Serikali ni 4 na mashirika ya dini, NGO's na binafsi ni 23. Vile vile, kuna Vituo vya Afya vya Serikali 5 na binafsi, Mashirika ya dini na NGO's 18. Zahanati zilizopo ni 67 za Serikali na 305 za binafsi/mashirika ya dini na mashirika yasiyo ya kiserikali. Hata hivyo, kuna upungufu wa Hospitali 4, vituo vya afya 25 na zahanati 48 ili kukidhi mahitaji ya idadi kubwa ya watu waliopo Mkoani.
|