Karibu katika Tovuti ya Mkoa wa Dar es Salaam, Jiji kubwa kuliko yote Tanzania ambalo ni Kitovu cha Shughuli za Serikali za Kiutawala, Viwanda, Biashara,Utalii na Shughuli za kibenki, pia ni Makao Makuu ya Balozi za nchi na Wakala mbalimbali wa Kimataifa. Mkoa unapakana na Mkoa wa Pwani kwa pande za Kaskazini, Magharibi na Kusini Magharibi,
Bahari ya Hindi ndiyo mpaka wa Mkoa kwa upande wa Mashariki na Kusini Mashariki.
Mkoa wa Dar es Salaam ni miongoni mwa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambazo zimefanya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru. Madhimisho haya yamefanyika tarehe 9-12 Oktoba,2011 katika viwanja vya Mnazi Mmoja-Jijini D' Salaam.
Maadhimisho hayo yaliambatana na maonyesho katika mabanda mbalimbali kutoka katika Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Wanachi pia walipata nafasi ya kuhudhuria maadhimisho haya pia kutembelea mabanda mbalimbali na kujionea mafanikio kwa kipindi cha miaka 50 ya uhuru (1961-2011
Mgeni Rasmi katika maadhimisho haya alikuwa Mhe. William V. Lukuvi (MP)-Waziri wa nchi Sera na Uratibu(Siku ya Ufunguzi) na Mhe. George H. Mkuchika (MP)- Waziri wa Nchi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Siku ya Kilele cha maadhimisho hayo).
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni: “Tumeweza, Tumethubutu, Tunasonga mbele”. “
Bonyeza hapa kusoma zaidi juu ya habari hii ...
Mkoa wa Dar es Salaam waadhimisha miaka 50 ya Uhuru
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni miongoni mwa Taasisi za umma zilizofanya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru. Madhimisho haya yamefanyika, katika viwanja vya Mnazi Mmoja - Jijini D' Salaam