Karibu katika Tovuti ya Mkoa wa Dar es Salaam, Jiji kubwa kuliko yote Tanzania ambalo ni Kitovu cha Shughuli za Serikali za Kiutawala, Viwanda, Biashara,Utalii na Shughuli za kibenki, pia ni Makao Makuu ya Balozi za nchi na Wakala mbalimbali wa Kimataifa. Mkoa unapakana na Mkoa wa Pwani kwa pande za Kaskazini, Magharibi na Kusini Magharibi,
Bahari ya Hindi ndiyo mpaka wa Mkoa kwa upande wa Mashariki na Kusini Mashariki.
Katika maadhimisho ya siku ya Wanawake mwaka huu Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ilipewa heshima ya kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani Kimkoa.
Maadhimisho haya yalifanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers-Kawe. Mgeni rasmi siku ya kilele alikuwa Mhe. Mkuu wa Mkoa Saidi Meck Sadiki.
Maadhimisho ya Kimkoa yalianza tarehe 6/03/2013 hadi 08/03/2013.
sambamba na maadhimisho haya kulikuwepo na
maonesho ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na wanawake wajasiriamali
Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 08 Machi. Kauli mbiu ya mwaka huu ni: “Uelewa wa Masuala ya Jinsia katika Jamii; Ongeza kasi”.
Bonyeza hapa kusoma zaidi juu ya habari hii ...
Wanachama wa kikundi cha 'FEDERATION ' wapata Msaada
Kampuni ya HSC kupitia mwakilishi wao Bw. Mohamed Abdallah, imekabidhi jumla ya mifuko 300 ya saruji kwa Umoja wa wanajamii wa'FEDERATION' huko Chamazi katika Halmashauri ya Manispaa y a Temeke.