Karibu katika Tovuti ya Mkoa wa Dar es Salaam, Jiji kubwa kuliko yote Tanzania ambalo ni Kitovu cha Shughuli za Serikali za Kiutawala, Viwanda, Biashara,Utalii na Shughuli za kibenki, pia ni Makao Makuu ya Balozi za nchi na Wakala mbalimbali wa Kimataifa. Mkoa unapakana na Mkoa wa Pwani kwa pande za Kaskazini, Magharibi na Kusini Magharibi,
Bahari ya Hindi ndiyo mpaka wa Mkoa kwa upande wa Mashariki na Kusini Mashariki.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. William V.Lukuvi kwa niaba yake binafsi na kwa niaba ya viongozi wa Halmashauri zote za Mkoa akipokea msaada wa mapipa 70 ya taka yenye thamani Tshs. 20,000,000/= kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Masoko wa Kampuni ya Twiga Cement Bwana Kigu Emmanuel .
Pamoja na msaada huu, Twiga Cement wamejitolea kukusanya taka hizi na kuzipeleka dampo kwa gharama ya Tshs.24,000,000/= kwa mwaka.
Kampuni ya Twiga Cement imekuwa ya kwanza kuchangia kati ya Wadau walioowaombwa msaada;
Mgao wa mapipa utagawanywa katika Halmashauri kwa mchanganuo ufuatao: Halmashauri ya Manispaa ya Ilala mapipa 30, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni mapipa 25, Halmashauri ya Manispaa ya Temeke mapipa 15 Bonyeza hapa kusoma zaidi juu ya habari hii ...
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika ngazi ya Vitongoji, Vijiji na Mitaa umefanyika mwezi Oktoba 2009,
chini ya Sheria
ya Uchaguzi ya mwaka 2002
na kanuni za Uchaguzi
za mwaka 2004 .